Deutsch English Kiswahili enkaina-e-retoto "mikono saidizi"
 
home
sisi ni nani
maarifa zaidi
maonesho ya picha
miradi yetu
dawa za asili
duka letu
washirikaji wetu/Links
mawasiliano
maoni yenu

Karibuni sana kwenye ukurasa wetu wa intaneti

Jina la „enkaina-e-retoto“ yaani „mikono saidizi“ ni jina la kikundi cha marafiki, ambao wapenda sana kuwasaidia wamasai na utamaduni wao kwa kushirikiana nao wenyewe na kuwaunga mkono…
… kwa habari zaidi tazama "sisi ni nani"

Mabadiliko ya hali ya hewa po pote duniani/pamoja na hali za ukame ambazo hutokea zaidi na zaidi duniani zinadhuru hata kabila fahari la wamasai. Maradhi ya mifugo, pengine matatizo ya kiekolojia zinawashawishi wamasai waache zaidi na zaidi namna ya utamaduni wao ya zamani. Wamasai wanatafuta njia za kujipatia nafuu kwa kushirikiana na maafisa wenyeji na mashirika ya misaada mbalimbali. Lakini jitihada yoyote ile kama vile ardhi ya pori ya wamasai itumike zaidi kwa ukulimo fulani huletea hata matatizo mengine kadha na husababisha madhara kwa namna wamasai walivyozoea kuishi tena madhara mabaya kwa mazingira yao...
… kwa habari zaidi tazama "maarifa zaidi"

Hali ya njaa ama hali ya kutopata malisho yaliyo kamili ambayo inatokana na ukame na shida zingine, inasababisha magonjwa  mbalimbali yanayodhoofisha hasa wale wasio na uwezo miongoni mwa jamii ya kimasai, kama vile akina mama na watoto wao. Mashirika na serikali ya Tanzania kwa kujenga hospitali na vituo vya matibabu, zinajitahidi sana kuboresha uhudumu wa afya kote nchini. Lakini wamasai kwa kulingana na mila yao wamezoea kutumia dawa za mitishamba hasa. Kutokana na jitihada za wamasai wenyewe, tena kwa  kushirikiana nao wenyewe katika miradi yenye malengo maalumu - kikundi chetu kiitwacho "enkaina-e-retoto" kinataka kuwaunga mkono wamasai hata  katika kazi ya kujenga vituo vya matibabu ambapo dawa za asili mbalimbali zitokanazo ulimwenguni popote zitapatikana, na vilevile yapatikanapo madawa yanayokunsanyika na kutengenezwa umasaini yenyewe…
… kwa habari zaidi tazama "miradi yetu"

Wamasai ndio wataalamu wenyewe hasa kuhusu dawa za mitishamba na utengenezaji wa chai asili kutokana na majani na mimea maalumu inayostawi katika baadhi ya sehemu umasaini. Wamasai huvuna mizizi ama majani hayo ya chai aslili kwa uanghalifu na bila uharibifu wa mazingira na wanakubali kuuzia mavuno hayo kupitia kikundi chetu cha "enkaina-e-retoto", ili yapatikane hata katika nchi za ng'ambo kama vile huko Ulaya n.k. …
… kwa habari zaidi tazama "dawa za asili"

Wamasai ni kabila lenye ufahari maalumu, na wasiokubali ushindi wa kuendeleza mila yao utegemee hasa na misaada na neema kutoka kwa nchi tajiri pekee, bali wajitegemee zaidi na uwezo wao wenyewe. Kama ilivyo ni kawaidha kwa makabila wanaotimiza utamaduni wao wa asili, hata wanawake wengi wa kimasai ni wataalamu wenye vipaji maalumu kwa kutengeneza kwa mikono mapambo mbalimbali ya kimila. Kwa nia hiyo ya kiujitegemea wenyewe, baadhi ya wanawake wa kimasai wanaoishi katika wilaya ya Simanjiro wanatengeneza wenyewe baadhi ya mapambo maalumu, kama vile mikufu, shanga na bangili za ngozi kwa kutumia vitu asili na shanga za rangi mbalimbali, ili wapate kuuzia kupitia kukundi chetu cha „enkaina-e-retoto“…
… kwa habari zaidi tazama "duka letu"

„enkaina-e-retoto“ ni kikundi cha watu wasiokuwa na upendeleo na makanisa wala madhebehu fulani na hakuna ushirikiano maalumu na watu wa dini yoyote. Bali sisi tunapenda kuwaunga mkono tukiwa marafiki wa wamasai na utamaduni wao. Vilevile tunayo nia ya kushirikiana kwa njia ya amani pamoja na makabila mengine waishio Tanzania/Afrika ya Mashariki, ili nao wanufaike pia kutokana na miradhi yetu kadhaa. Miradi yetu inayo malengo ya kupambana na njaa/umasikini, pengine miradi yetu hulingana na matumaini makuu ya mamlaka ya mbuga za wanyama zilizo karibu, yenye nia ya kuhifadhi mimea ya asili na wanyama pori  - na kwa hivyo miradi yetu ni muhimu mikoani na hata kwa mambo ya taifa...
… kwa habari zaidi tazama "washirikiaji wetu/Links"

Unayo maswali mengine ama mapendekezo fulani. Ama unapenda kubadilishana mawazo kuhusu mambo yetu ya kuwaunga mkono wamasai, ama ukipenda kusaidia kikundi chetu cha „enkaina-e-retoto“ kwa njia yoyote ile…?
… kwa habari zaidi tazama "mawasiliano"

copyright by massailand.com